Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni

Tunaipa Uhai wa Kisheria Biashara yako

Huduma Zetu

UTOAJI WA LESENI ZA VIWANDA

Kiwanda ni nini?

Ni shughuli inayohusisha uzalishaji kwa kubadilisha malighafi kuwa bidhaa au

muundo wa kitu kinachofaa kwa matumizi.

Aina za Viwanda

  1. Viwanda vidogo – hivi huwa na kiasi cha uwekezaji kisichozidi Sh.100,000,000/-
  2. Viwanda vikubwa – hivi huwa na kiasi cha uwekezaji kinachozidi Sh. 100,000,000/-

Faida za kusajili/kuwa na leseni ya kiwanda ni zipi?

  1. Kutambulika na taasisi za fedha kama vile benki (wakati wa kufungua akaunti).
  2. Kupata mikopo katika taasisi za fedha kama benki.
  3. Kuongeza wigo wa kupata kazi na zabuni mbalimbali.

Nyaraka za kuambatisha

  1. Mchanganuo wa mradi
  2. Uthibitisho wa mahali kilipo kiwanda
  3. Fomu ya majumuisho (consolidated form)

Hatua 10 za kusajili kiwanda

  1. Tembelea www.brela.go.tz au ors.brela.go.tz
  2. Ingia katika akaunti yako ya usajili kwa njia ya mtandao (ORS) au tengeneza akaunti katika mfumo.
  3. Chagua huduma mtandao.
  4. Chagua leseni ya kiwanda.
  5. Chagua aina ya huduma.
  6. Jaza kiasi cha uwekezaji.
  7. Jaza taarifa za kiwanda husika.
  8. Pakia viambatisho katika mfumo.
  9. Lipa kwa njia ya simu au benki.
  10. Maombi yatafanyiwa kazi baada ya malipo kupokewa.